Showing posts with label UDAKU SPESHO. Show all posts
Showing posts with label UDAKU SPESHO. Show all posts

Monday, June 17, 2013

Allen Iverson’s Ex-Wife Accuses Him Of Kidnapping Their Children

allen-iverson-kids-378x402
When it rains, it pours, and there is no um-br-ella in sight for A.I.
Former NBA star Allen Iverson has abducted his own children … so says his ex-wife, and now she’s begging the court to force Allen to give them back.
Tawanna Iverson just filed legal docs, claiming Allen recently asked for permission to take their five kids on a short vacation to Charlotte, NC from May 22nd-May 26th (and Tawanna agreed) but when May 26th rolled around, the children hadn’t been returned.
The kids range in age from 3 to 16 years old.

LOVE SIPATI-NEY WA MITEGO


Baada ya kufanya poa sana na ngona ya Muziki gani Ney wa Mitego akiwa na Diamond Platnum mkali huyo alielamba tuzo ya Kili Music Awards kwa wimbo Bora wa Hip -Hop ameachia ngoma nyingine inayokwenda kwa jina la Love Sipati akiwa ameimpa shavu Sheby.

Katika ngoma hilo ambalo mkali wa Hip Hop amelalama kwa kuimba limefanywa na mtu mzima Nas Bussiness katika Studio ya Pamoja Records.

Ney wa mitego amekuwa msanii wa kwanza kuiwakilisha vizuri Manzese kwa kurudisha Tuzo kwa mwaka huu pande hizo.

Monday, June 3, 2013

PICHA YA SIKU BOB JUNIOR AKIWA NA MWANAE,

KATIKA POZI NI BOB JUNIOR AKIWA NA MWANAE KIPENZI ATAKAE RIDHI MIKOBA YA URAISI WA MASHAROBARO BAADA YA MZAZI KUIWEKA PEMBENI SIKU ZA USONI.

HUU NI MFANO WA KUIGWA KAMA MZAZI KUTUMIA MUDA WAKO KUREA MWANAO NA SI KUWAKIMBIA NA KUSABABISHA WATOTO WASIO NA MAKOSA KUISHI KWA SHIDA NYINGI

MPAKA HAPO UMEKATA MANENO YA WATU WALIOKUTUPIA MANENO MACHAFU HAPO UMEONESHA WANAUME WAKO

BIG UP BOB JUNIOR

Thursday, May 30, 2013

COW BOY NJOO UONE SIMANZI YA TAIFA JUU YAKO-MRISHO MPOTO



Msanii maarufu wa miondoko ya Kughani Mrisho Mpoto anaefahamika kwa jina la Mjomba Jana alipofika katika Msiba wa Msanii Mwenzake Maeneo ya Mbezi Beach akionekana kushikwa na Uchungu alipoona namna Sauti za Wazee kwa Watoto wakilia kwa uchungu baada ya kumpoteza Kijana wao mpendwa aliefariki siku ya Tarehe 28 huko nchini South Afrika.

hata uwe na roho ngumu kama mpingo, ukifika nyumba hii utalia tu, ukisikia sauti za wazee na watoto zikipokezena kulia kwa uchungu.. unaweza kusema neno likamchukiza mungu!. cow boy njoo uone simanzi hii ya kitaifa juu yako”

Mrisho Mpoto alifika Msibani hapo kuwafariji ndugu jamaa na Marafiki walioguswa moja kwa moja na msiba huo na baada ya kusaini Kitabu cha Wageni na kwenda kuketi ndipo alipotafakari na kuona watu walikuwa na mapenzi na Albert kwani wengi wao walikuwa wakilia kwa uchungu mkubwa kutokana na kifo cha Kijana huyo kuwa ni cha Ghafla.

Mwili wa msanii Albert Mangwear unatarajiwa kusafirishwa siku ya Jumamosi kutoka nchini South Afrika na kuletwa Tanzania kwa maandalizi ya maziko yatakayofanyika Mjini Morogoro.

MRISHO MPOTO AKISAINI KITABU CHA WAGENI JANA MSIBANI MBEZI 

AFUNGWA MWAKA MMOJA BAADA YA KUTUMA SMS MBAYA KWA WAZIRI



Mkazi Wa Mburahati Jogoo jijini Dar es salaam, Nassor Issa Mohamed(25) amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja au kulipa faini ya shilingi milioni tatu kwa kosa la kuwatumia ujumbe wenye nia mbayawa simu ya mkononi Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt.Emmanuel Nchimbi na Inspekta General wa Polisi Said Mwema.

Akitoa hukumu hiyo hakimu Helen Riwa wa mahakama Kisutu aliiambia mahakama kuwa Mohamed alisajili kadi zake za simu kwa majina tofauti na kwa mitandao tofauti kwa nia ya kutumia kadi hizo kutuma ujumbe wa simu wenye nia mbaya kwa viongozi hao.


Alisema mshtakiwa alikutwa akiwa na kadi ya simu yenye namba 0759 799956 ya Vodacom iliyosajiliwa kwa jina la Fadhil Issah, nyingine ya Airtel 0687 521948 iliyosajiliwa kwa jina la Godfrey Joseph na kadi yenye namba 0687521947 ya Airtel iliyosajiliwa kwa jina la Fadhil Issa.


Hakimu Riwa aliitaka jamii kutumia kwa uangalifu mitandao kwa kuwani teknolojia mpya ambapo makosa yake yanakuwa ni mapya na sheria ni mpya.


Alisema ametoa adhabu hiyo kwa kutumia Sheria ya Mawasiliano ya kielektroniki na Posta (EPOCA) ya mwaka 2010 kifungu cha 132 ili iwe fundisho kwa wote wenye nia ya kufanya makosa kama hayo.


Awali Mwendesha Mashitaka Ladislaus Komanya aliiambia mahakama kuwa mnamo Mei 20 mwaka huu taarifa za kiinteligensia zilifikishwa kwa Maafisa wa juu wa jeshi la Polisi kuwa kuna mtu aliyesajili simuzake kwa mitandao tofauti anatumia simu hizo kuwatumia ujumbembaya wa simu ya mkononi Waziri Nchimbi na IGP na baada ya upelelezi ilipobainika kuwa namba hizo zilikuwa zimesajiliwa kwa majina tofauti.


Alisema iligundulika kuwa namba hizo zilikuwa zinamilikiwa na mtuhuyo ambaye jina lake halisi ni Nassor Issah Mohamed


Alisema Mohamed alikamatwa Mei 25mwaka huu na baada ya mahojiano alikiri kumiliki kadi ya simu na kwamba ndiyo yeye aliyesajili namba hizo kwa mitandao tofauti akitumia majina tofauti ili kuficha utambulisho wake akiwa na lengo lakufanya uhalifu. Mshtakiwa alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Mei 27 mwaka huu na kukiri mashitaka.



SIJAWAHI KUMPIGA NGWEAR ALIPO ANAJUA-CHID BENZ



Msanii wa Hip Hop Bongo anewakilisha kipande cha Ilala ChiD Benz amefunguka leo na kusema kuwa hakuwahi kumpiga Marehemu Ngwear kama ambavyo amekuwa akikariliwa na baadhi ya vyombo vya Habari kuwa amewai kumpiga mwanamuziki huyo enzi za Uhai wake.

Chid amesema kuwa hizo stori watu wanapozizungumzia zinamuumiza moyo wake na kumtesa pia na madai yake amesema kuwa kwa mara ya mwisho alizungumza na Ngwear kwa njia ya Sms japo hakuona ulazima wa kuliweka wazi.

'Story za kumpiga marehem zinaniumiza kwa kweli,mara ya mwisho alinitumia msgs na tukaongea sio lzm tuseme.SIJAWAI KUMPIGA NGWEA alipo anajua”

Chid Benz ameonesha kuumizwa na maneno ya kuwa aliwahi kumpiga Marehemu na ndio maana anajaribu kuwaambia watu kuwa hakufanya kitendo hicho na kusema ya kuwa alipo Marehemu anatambua ya kuwa hajawai kufanya kitendo hicho.

Tuesday, May 28, 2013

JERRY SILAA AUMIZWA NA CHEMBA SQUAD



Mwanasiasa na Mayor wa Manispaa ya Ilala Mh Jerry Silaa ameonesha kuumizwa kwa kupotea kwa kundi la Muziki wa bongo fleva Chemba Squad lililokuwa likifanya poa katika tasnia ya muziki wa Bongo Fleva miaka kadhaa ya nyuma.

Silaa ameoneshwa kuumizwa na ukimya wa wanamuziki hao kwa sasa ingawa ameonesha kukumbuka mambo mengi ya nyuma baada ya kuonana na member mmoja ofisini kwake ambae ni Noorah

Just met Nurah in my office, amenikumbusha mbaaali! Chemba squad! Maisha haya! Sad, simsikii sana”


Kundi la Chemba Squad liliundwa na wakali kama Gwair Cow Boy,Noorah a.k.a Babastlyz,Mez B mzee wa Kikuku pamoja na Dark Mastar na kufanya poa sana kwa ngoma zao kama kundi na ngoma zao kama mtu mmoja mmoja katika kundi.

Noorah siku za karibuni alitoa wimbo wake mpya uliokwenda kwa jina la Nikupe nini alimshirikisha Msanii Ally Kiba 4 real na kufanya poa katika radio mbalimbali hapa town.




DR CHENI ALISHWA SUMU,LULU AHAHA HOSPITALI


Katika hali ya kushangaza na isiyo eleweka mwigizaji Mahsein Awadhi maarufu kama Dr. Cheni amekumbwa na balaa la kulishwa chakula chenye sumu weekend iliyopita alipokuwa kwenye sherehe moja ya harusi jijini Dar es Salaam alipohudhuria kama MC au mshereheshaji wa harusi hiyo.

Akiongea leo asubuhi, Dr. cheni alisema kuwa baada ya kumaliza kula chakula ambacho alipakuliwa na mmoja wa wahudumu wa sherehe hiyo alianza kujisikia vibaya na kuishiwa nguvu na aliamua kutoka nje kujaribu kupata hewa akidhani ladba ni joto la ukumbini ila hali ilizidi kuwa mbaya na aliamua kutafuta maziwa akihisi labda inaweza kuwa vidonda vya tumbo ndipo alipoanza kutapika na baadae kukumbizwa hospitalini na ndipo alipogungulika kuwa amelishwa chakula chenye sumu.

Tulipomuuliza labda sababu gani anahisi zinaweza kuwa zimepelekea watu hao kutaka kumdhuru alisema kuwa, mpaka sasa hajaweza kupata jibu kamili ila anaamini watu waliofanya hivyo wanamfahamu na wana nia mbaya sana kwake na sio watu wema.

Dr. Cheni alisema kuwa kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na moja ya watu walikuwa wa kwanza kufika hospitalini baada ya yeye kupatwa na majanga hayo ni mwigizaji Elizabeth Michael (LULU) ambaye kwa sasa yupo karibu sana na Dr. Cheni aliyekuwa mstari wa mbele katika kushughulikia mpaka kufanikisha suala la dhamana ya kesi iliyokuwa inamkabili mwanadada huyo.
Source:Swahili Tz

Sunday, May 26, 2013

LADYA JAYDEE KUJUA HATMA YAKE LEO


Mwanamuziki Lady Jaydee Leo atajua hatima yake katika mahakama ya Kinondoni kufuatia kufunguliwa kesi ya madai dhidi yake na viongozi wa Radio wa Redio ya Clouds Fm.
Wiki kadhaa zilizopita mwadada huyo aliitwa mahakamani hapo na kuzuiliwa kuzungumza jambo lolote lile kuhusiana na hao watu waliofungua kesi dhidi yake na hakupaswa kuzungumzia jambo lolote lile juu ya Mgogoro walionao mpaka siku ya leo mahakama itapo toa kauli yake juu ya jambo hilo.
Kwa mujibu wa Lady jaydee anatakiwa kufika Mahkama ya Kinondoni kuanzia Mida ya saa Mbili na Nusu kwa ajiri ya kwenda kusikiliza nini kinaendelea juu ya sakata hilo.


Friday, May 24, 2013

SLAA:SIMCHUKII JK KWA DINI YAKE.BALI UTENDAJI KAZI WAKE



Katibu Mkuu wa Chadema,Dk Willbroad Slaa amedai kuwa anachukia udhaifu wa utendaji kazi wa Rais Jakaya Kikwete,kama kiongozi mkuu wa nchi na katu hamchuki kutokana na dini yake kama watu wengine wavyopotosha.

Dk Slaa aliyasema hayo jana kwenye maeneo ya Riroda, Galapo,Mwada,Magara,Magugu,Mutuka,Sendo na Mamire,wilayani Babati,mkoani Manyara na kudai kuwa hatanyamaza kamwe kwa kuwa wananchi hawatendewi haki na matumaini yao yanaminywa na watawala.
Alisema hatamung’unya maneno wala kusita kuendelea kusema udhaifu wa Rais Kikwete hasa katika kushindwa kuchukua au kufanya uamuzi sahihi na kwa wakati sahihi kwa sababu matokeo yake yanaathiri Watanzania wote ambao yeye pamoja na chama chake wamejitolea kuwa wasemaji wao.
Nchi hii inavunjwa,napambana na Kikwete kwa sababu ni dhaifu,” alisema na kuongeza:
Kuna watu wanapotosha jambo hili,mimi sina chuki na Rais Kikwete kwa sababu ya dini yake”. Alisema.
Source Mwanachi.


UHURU SELEMAN-NICHEZE TIMU GANI MSIMU UJAO?



Kiungo mshambuliaji kutoka Timu ya Azam Fc alimaarufu kam Uhuru Seleman Mwambongo baada ya kumaliza msimu wa Pili wa Ligi kuu bara akiwa na Timu ya Azam Fc amewataka mashabiki wake wamchagulie timu ya kwenda kucheza msimu ujao huku akiwa ametaja timu nne tu Simba Sc,Coastal Union.Azam Fc na Tusker Fc.
Leo ni Tarehe 24 May nisiku ambayo namaliza miezi sita ndan ya Azam ... Na nakupa nafasi wewe kama shabiki wangu kuchagua msimu ujao nicheze timu (gani) vigezo na hekima .... 1.Simba sc .2.Coastal 3.Azam fc 4.tusker fc”
Mbali na kuwapa vigezo hivyo mashabiki wake lakini amewaomba kutumia hekima katika kumshauri acheze timu ipi,nilipofanya utafiti wangu nikagundua kuwa mashabiki wengi wa Simba Fc walimtaka Uhuru arejee nyumbani kwa kujiunga na timu hiyo aliyokwisha ichezea kipindi cha nyuma kabla ya kujiunga na Azam Fc,na yeye alikili hilo na kusema kuwa wengi wape.

Kwa mtazamo huo inawezekana msimu ujao uhuru akalejea kuichezea timu ya Simba Sc kwani ameonesha mapenzi hayo dhahiri kwanza kwa kuipa nafasi ya kwanza katika list ya timu alizozitaja pili katika list hiyo hajaitaja kabsa Yanga hivyo inawezekana hawajaonesha uitaji au laah hajapenda kuungana na timu hiyo.


Thursday, May 23, 2013

PICHA ZA SIKU ENJOY IT


BEN PAUL AKIWA NA DICKSON MSAMI

BEN PAUL AKIWA NA MPITA NJIA

AFANDE SELE  AKIWA NA RAISI WA WANAFUNZI 

NYALIFA,AFANDE SELE,MBUMI AND DICKSON MSAMI

BEN PAUL AKICHAT NA FANS ZAKE HUKU WATOTO WAZURI WAKIMPA SUPPORT

PAMOJA TUNAWAKILISHA

BEN PAUL AKISALIMIANA NA AFANDE SELE