Msanii
maarufu wa miondoko ya Kughani Mrisho Mpoto anaefahamika kwa jina la
Mjomba Jana alipofika katika Msiba wa Msanii Mwenzake Maeneo ya Mbezi
Beach akionekana kushikwa na Uchungu alipoona namna Sauti za Wazee
kwa Watoto wakilia kwa uchungu baada ya kumpoteza Kijana wao mpendwa
aliefariki siku ya Tarehe 28 huko nchini South Afrika.
“hata
uwe na roho ngumu kama mpingo, ukifika nyumba hii utalia tu, ukisikia
sauti za wazee na watoto zikipokezena kulia kwa uchungu.. unaweza
kusema neno likamchukiza mungu!. cow boy njoo uone simanzi hii ya
kitaifa juu yako”
Mrisho
Mpoto alifika Msibani hapo kuwafariji ndugu jamaa na Marafiki
walioguswa moja kwa moja na msiba huo na baada ya kusaini Kitabu cha
Wageni na kwenda kuketi ndipo alipotafakari na kuona watu walikuwa na
mapenzi na Albert kwani wengi wao walikuwa wakilia kwa uchungu mkubwa
kutokana na kifo cha Kijana huyo kuwa ni cha Ghafla.
Mwili
wa msanii Albert Mangwear unatarajiwa kusafirishwa siku ya Jumamosi
kutoka nchini South Afrika na kuletwa Tanzania kwa maandalizi ya
maziko yatakayofanyika Mjini Morogoro.
![]() |
MRISHO MPOTO AKISAINI KITABU CHA WAGENI JANA MSIBANI MBEZI |
0 comments:
Post a Comment