Thursday, May 30, 2013

STANLEY MSUNGU AILAUMU KAMATI YA MAZISHI


Msanii wa Filamu Nchini Tanzania Stanley Msungu jana amenukuliwa akitoa lawama kwa kamati ya mazishi ya Msanii Ngwear kwa kutofanyia vikao vyao Msibani.

kikawaida kamati za mazishi hufanya vikao vyao msibani sasa kamati ya mzishi ya ndugu yetu ngwea hatuielewi mnafanyia wapi vikao vyenu? tunaona taarifa tu kwenye mitandao lakini msibani hatuwaoni mda huu mnafanyia wapi vikao?”

Kitendo cha Kamati ya mazishi kutofanyia Vikao hivyo Msibani kumepelekea Baadhi ya watu kuona hakuna ulazima wa kufika nyumbani moja kwa moja wakati kuna wafiwa wanahitaji Faraja kutoka kwetu pindi watuonapo wanafarijika kuona tupo pamoja nao.

Kwa mujibu wa Stanley majira ya saa Saba Mchana Jana Msibani kulikuwa na watu wachache sanaa na Wasanii waliofika kwa kipindi ambacho yeye alikuwepo ni Kara jeremiahar pamoja na Mrisho Mpoto,na akatoa rai kwa wasanii wenzake kufika Msibani ili kuwafariji wafiwa waliopo katika wakati mgumu huu.

kiukweli watu ni wachache sana, tangu nimefika tena leo saa saba mchna hatufiki 20 na wasanii waliofika tangu mimi nipo hapa mpaka mda huu hasa ukinitoa mimi na mdogo wangu noster ni kala jelemiah na mrisho mpoto najua wenda walikuwepo wakati mimi sipo wameondoka lai yangu tuje msibani ndugu zangu tuwajibike na kila kinachoendelea”

BWANA AMETOA BWANA AMETWAA.



0 comments:

Post a Comment