Thursday, May 30, 2013

BUSHOKE AFUNGUKA KWA WALE WALIOPIGA PICHA MWILI WA MAREHEMU


Msanii Bushoke alietamba miaka ya nyuma na Ngoma zake kibao kama Watashindwa lala,Dunia Njia na zingine kibao ambapo kwa sasa amehamishia makazi yake Nchini South Africa,ameonesha kukerwa na baadhi ya waandishi wa Mitandao ya Kijamii pamoja na na wale waliopo katika vyombo vya Habari kwa vitendo vya kupotosha jamii na kutokuwa na utu miyoni mwao.

Msanii huyo amefunguka hayo jana baada ya kuona na kusoma ripoti iliokua ikisambazwa katika vyombo vya habari ikieleza chanzo cha kifo cha Msanii Ngwear,kwa mujibu wa Bushoke amesema kuwa ile ripoti haikutolewa na madaktari kutoka katika Hospitali aliokuwa amelazwa marehemu bali ni mtu tu aliunda na kuitawanya ili aweze kupata wasomaji wengi katika Blog yake au gazeti lake.

Vile vile Bushoke alioneshwa kukerwa na kitendo cha mtu aliepiga picha mwili wa marehemu wakati wapo katika chumba cha kuifadhia Maiti akiwa bado hata ajaandaliwa,amedai kuwa kitendo hicho ni sawa ni kumkosea marehemu na kuendelea kumfedheesha na kuikosea familia,ndugu na rafiki wa marehemu.

kiukweli nikekerwa sana na Mtu aliepiga picha ya mwili wa marehemu kwani ni kuendelea kuiumiza familia,Ndugu na Marafiki wa marehemu,sijui lengo lake lilikuwa nini wakati sisi tulipiga marufuku kupiga picha pale lakini yeye kapiga picha Mwili wa Marehemu ukiwa hata haujaandaliwa,hili jambo si ungwana na si haki kabsa,akumbuke Dunia tunapita tuu.




0 comments:

Post a Comment