Wednesday, November 13, 2013

STEVE WA YANGA 'NIMEKUBALI KUOLEWA'

Alianza kupata umaarufu baada ya kuonesha Mapenzi makubwa aliyonayo katika Timu yake ya Soka ya Yanga kwa kulia huku akionesha machungu makubwa
aliyokuwa nayo baada ya Timu yake hiyo kukubali kichapo Mabao Matano kutoka kwa Watani wao wa Jadi Simba.

Kutokana na watu wengi kupenda aina ya Mapenzi aliyonayo katika Timu yake hiyo ndipo jamii ilianza kumtambua Steve wa Yanga kupitia Interview ambayo alifanya na Mtangazaji Millard Ayo kupitia Mtandao wake wa Jamii.

Interview hiyo ilizidi kuongeza Umaarufu na kulipaisha zaidi jina la Steve wa Yanga mpaka huko Nchini Kenya ambapo kuna Kituo cha Tv kilifunga Safari kuja Tanzania na kutengeneza naye Documentary ambayo nayo ilizidi kumvusha boda na kumuongezea idadi kubwa ya Mashabiki ambao wengi wao huangua kicheko kutokana na namna alivyona mapenzi ya Kweli ya Club yake ya Yanga.

Salama Jabir kupitia Mkasi Show ambayo inaruka katika Ting'a Namba moja kwa vijana alimuona Steve na kumpa Shavu tena na hii ilitokana na kukutana na kijna Steve wa Yanga alipokwenda katika Usaili wa Epiq Bongo Star Search 2013 alipokwenda kuonesha kipaji chake kingine cha Kuimba mbali na kutoa mchozi.

Kutokana na kuonekana katika Misukosuko na mihangaiko hiyo Dr Chein Muingizaji akaona kipaji cha Steve wa Yanga na kuamua kuigiza naye katika Filamu yake inayokwenda kwa Jina la NIMEKUBALI KUOLEWA ambapo katika Filamu hiyo mkali Steve wa Kulia amepewa scene ya Kumwaga mchozi pia.

Je unatka kujionea kipande hicho BOFYA HAPO NA MTIZAME MWENYEWE.

0 comments:

Post a Comment