Mahakama
ya Hakimu Mkazi Arusha, imewazuia wafanyakazi 14 wa Benki ya
Exim tawi la Arusha, akiwamo meneja wa benki
hiyo, Bimal Gondalia,
kutosafiri nje ya mkoa wa Arusha, bila idhini ya Mahakama
hiyo,Maamuzi hayo yanawafanya washtakiwa kushindwa kusafiri au kutoka
katika Mji wa Arusha bila ruhusa ya Mahakama.
Washitakiwa
hao walipandishwa kizimbani Septemba 20, mwaka huu na kusomewa
shitaka la kula njama na kuiba zaidi ya Sh. bilioni saba.
Washitakiwa
wenyewe ni Joyce Kimaro, Lilian Kageye, Doroth Chijana, Tuntufe
Agrey, Michael Majebele, Ginese Massawe na Joseph Meck.
Wengine ni Robert Rubeni, Livingstone Mwakijabe, Clara Lawena, Evance Kashebo, Neema Kinabo na Christopher Lyimo.
Pia wanadaiwa kuiibia benki hiyo Dola za za marekani 400,000 katika kipindi cha miaka mitatu.
Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Diaz Makule, alidai kuwa wizi huo ulifanywa na wafanyakazi hao kwa nyakati tofauti kati ya mwaka 2011 na 2013.
Wengine ni Robert Rubeni, Livingstone Mwakijabe, Clara Lawena, Evance Kashebo, Neema Kinabo na Christopher Lyimo.
Pia wanadaiwa kuiibia benki hiyo Dola za za marekani 400,000 katika kipindi cha miaka mitatu.
Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Diaz Makule, alidai kuwa wizi huo ulifanywa na wafanyakazi hao kwa nyakati tofauti kati ya mwaka 2011 na 2013.
0 comments:
Post a Comment