Wednesday, September 25, 2013

WAKAZI WA KIGOGO LUHANGA WAKUTWA NA MAITI YENYE MADAWA YA KULEVYA TUMBONI.

Wanawake wawili wakazi wa Kigogo Luhanga Jijini Dar es Salaam waliofahamika kwa majina ya Nasra Omari (36) na Mwanaisha Kapama (36) walikutwa na maiti
iliyokuwa na dawa za kulevya aina ya heroin pipi 33 zenye thamani ya mamilioni ya fedha. 
Kamishna Kova alisema alipata taarifa kuwa kuna mtu aliyefahamika kwa majina ya Rajabu Kidunda na Mashaka Mabruki  (43) ambaye ni mfanyabiashara aliyefika Dar es Salaam kutoka mkoani Mtwara kwamba alifariki dunia ghafla muda mfupi baada ya kutoka bafuni kuoga.

Baada ya kufikishwa Hospitali walipoipasua maiti walikuta pipi hizo zenye urefu wa sentimita sita.

uchunguzi  unaonyesha kuwa marehemu alifika Dar es Salaam kutoka Mtwara Septemba 21 mwaka huu kwa maelezo kwamba alifika kwa ajili ya matibabu kwa kuwa alikuwa mgonjwa. 

Hata hivyo, mtu huyo alifariki siku hiyo hiyo aliyowasili jijini Dar es Salaam.

0 comments:

Post a Comment