Baada
ya Ngasa Mwenyewe kushindwa kulipa deni la Millioni 45 Kwa Club yake
ya Zamani ya Simba kama ambavyo Kamati ya Sheria na Hadhi za
Wachezaji ya
Shirikisho la Soka nchini (TFF),ilivyomtaka Ngasa
kuzilipa kama adhabu na kutocheza mechi sita msimu huu pamoja na
baada ya usajili wake kuleta utata kutokana na kujisajili klabu mbili
tofauti, Simba na Yanga.
Jana
Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alinukuliwa na vyombo vya
habari akisema kuwa, wapo tayari kumsaidia Ngasa kulipa deni hilo ila
kwa masharti mawili.
"Kwanza akubali kukatwa kiasi hicho kidogo kidogo katika mshahara wake hadi deni hilo litakapomalizika, au laah aridhie kuingia mkataba mwingine wa miaka mitatu," alinukuliwa Mwalusako.
"Kwanza akubali kukatwa kiasi hicho kidogo kidogo katika mshahara wake hadi deni hilo litakapomalizika, au laah aridhie kuingia mkataba mwingine wa miaka mitatu," alinukuliwa Mwalusako.
Mmoja
wa rafiki wa karibu wa Mchezaji huyo amesema kuwa Mpira ni Maisha ya
Mrisho ngasa hivyo hawezi kupingana ma maamuzi ya Club yake ya Yanga.
"Soka
ni maisha yake. Amesema hana ujanja wa kupindua uamuzi huo kwa kuwa
kinyume na kufanya hivyo, itamlazimu kuendelea kukaa benchi hadi
atakapolipa deni hilo la Simba kama alivyotakiwa kufanya na Kamati ya
TFF," alisema rafiki huyo huku akiomba hifadhi ya jina lake kwa
kuwa yeye si msemaji wake.
0 comments:
Post a Comment