Tuesday, May 28, 2013

JERRY SILAA AUMIZWA NA CHEMBA SQUAD



Mwanasiasa na Mayor wa Manispaa ya Ilala Mh Jerry Silaa ameonesha kuumizwa kwa kupotea kwa kundi la Muziki wa bongo fleva Chemba Squad lililokuwa likifanya poa katika tasnia ya muziki wa Bongo Fleva miaka kadhaa ya nyuma.

Silaa ameoneshwa kuumizwa na ukimya wa wanamuziki hao kwa sasa ingawa ameonesha kukumbuka mambo mengi ya nyuma baada ya kuonana na member mmoja ofisini kwake ambae ni Noorah

Just met Nurah in my office, amenikumbusha mbaaali! Chemba squad! Maisha haya! Sad, simsikii sana”


Kundi la Chemba Squad liliundwa na wakali kama Gwair Cow Boy,Noorah a.k.a Babastlyz,Mez B mzee wa Kikuku pamoja na Dark Mastar na kufanya poa sana kwa ngoma zao kama kundi na ngoma zao kama mtu mmoja mmoja katika kundi.

Noorah siku za karibuni alitoa wimbo wake mpya uliokwenda kwa jina la Nikupe nini alimshirikisha Msanii Ally Kiba 4 real na kufanya poa katika radio mbalimbali hapa town.




0 comments:

Post a Comment