Thursday, May 30, 2013

SIJAWAHI KUMPIGA NGWEAR ALIPO ANAJUA-CHID BENZ



Msanii wa Hip Hop Bongo anewakilisha kipande cha Ilala ChiD Benz amefunguka leo na kusema kuwa hakuwahi kumpiga Marehemu Ngwear kama ambavyo amekuwa akikariliwa na baadhi ya vyombo vya Habari kuwa amewai kumpiga mwanamuziki huyo enzi za Uhai wake.

Chid amesema kuwa hizo stori watu wanapozizungumzia zinamuumiza moyo wake na kumtesa pia na madai yake amesema kuwa kwa mara ya mwisho alizungumza na Ngwear kwa njia ya Sms japo hakuona ulazima wa kuliweka wazi.

'Story za kumpiga marehem zinaniumiza kwa kweli,mara ya mwisho alinitumia msgs na tukaongea sio lzm tuseme.SIJAWAI KUMPIGA NGWEA alipo anajua”

Chid Benz ameonesha kuumizwa na maneno ya kuwa aliwahi kumpiga Marehemu na ndio maana anajaribu kuwaambia watu kuwa hakufanya kitendo hicho na kusema ya kuwa alipo Marehemu anatambua ya kuwa hajawai kufanya kitendo hicho.

0 comments:

Post a Comment