Thursday, May 30, 2013

LADY JAYDEE AOMBA RADHI



Mwanamuziki Lady Jaydee anaetamba na kibao chake cha Joto Hasira katika vituo mbalimbali vya Radio na Luninga hapa nchini ameomba radhi kwa mashabiki wake kufuatia kuairisha show yake ya Miaka kumi na tatu kutokana na msiba uliotokea wa msanii Albert Magwear.

Show ya mwanadada Jide ilipaswa kufanyika siku ya Ijumaa ya kesho katika Ukumbi wa Nyumbani Lounge lakini jana kupitia kipindi cha Super Mix cha East Africa Radio alitangaza kusitisha show yake kupisha taratibu za msiba kwanza na kusema atatangaza siku baada ya msiba kuisha.

Tunaomba radhi kwa watu wote ambao mlikuwa mmeshanunua tickets za miaka 13 ya Lady JayDee ambapo onyesho ilikuwa lifanyike Ijumaa ya tar 31 May 2013.

Tunapenda kuwataarifu kuwa onyesho hilo limesitishwa kutokana na msiba mzito wa msanii mwenzetu Ngwair mpaka hapo tutakapo wataarifu tena”


Akizungumzia kwa wale waliokwisha nunua ticket teyari amesema kuwa wazitunze Tickets hizo kwani ndizo hizo zitakazo tumika siku ya show pindi itapotangazwa siku rasmi.

“Wale mliokwisha nunua tickets naomba mzitunze tickets zenu, kwani ndio hizo hizo mtakazozitumia siku ya show hata kama tarehe imebadilishwa.Natanguliza shukrani na naomba radhi kwa usumbufu wowote nitakaokuwa nimewasababishia,Kila kitu kitaendelea kama kilivyokuwa kimepangwa, hapo baadae”


0 comments:

Post a Comment