Friday, May 24, 2013

UHURU SELEMAN-NICHEZE TIMU GANI MSIMU UJAO?



Kiungo mshambuliaji kutoka Timu ya Azam Fc alimaarufu kam Uhuru Seleman Mwambongo baada ya kumaliza msimu wa Pili wa Ligi kuu bara akiwa na Timu ya Azam Fc amewataka mashabiki wake wamchagulie timu ya kwenda kucheza msimu ujao huku akiwa ametaja timu nne tu Simba Sc,Coastal Union.Azam Fc na Tusker Fc.
Leo ni Tarehe 24 May nisiku ambayo namaliza miezi sita ndan ya Azam ... Na nakupa nafasi wewe kama shabiki wangu kuchagua msimu ujao nicheze timu (gani) vigezo na hekima .... 1.Simba sc .2.Coastal 3.Azam fc 4.tusker fc”
Mbali na kuwapa vigezo hivyo mashabiki wake lakini amewaomba kutumia hekima katika kumshauri acheze timu ipi,nilipofanya utafiti wangu nikagundua kuwa mashabiki wengi wa Simba Fc walimtaka Uhuru arejee nyumbani kwa kujiunga na timu hiyo aliyokwisha ichezea kipindi cha nyuma kabla ya kujiunga na Azam Fc,na yeye alikili hilo na kusema kuwa wengi wape.

Kwa mtazamo huo inawezekana msimu ujao uhuru akalejea kuichezea timu ya Simba Sc kwani ameonesha mapenzi hayo dhahiri kwanza kwa kuipa nafasi ya kwanza katika list ya timu alizozitaja pili katika list hiyo hajaitaja kabsa Yanga hivyo inawezekana hawajaonesha uitaji au laah hajapenda kuungana na timu hiyo.


0 comments:

Post a Comment