Friday, May 24, 2013

NEY WA MITEGO,MADEE KUKINUKISHA TMK JUMAPILI HII.


Katika ule mpango wa kuhakikisha vijana wanashika Mic na kuchana mistari yao na kuonesha vipaji vyao kupitia Marcho Chali Foundation unaokwenda kwa jina Epic Open Mic wasanii kama Diamond Platinum,Madee,Ney wa Mitego na Godzillah wataonesha uwezo wao bure katika viwanja vya Mwembe Yanga pande za Temeke Jumapili hii.

Kwa mujibu wa Marcho Chali amesema kuwa lengo la Epic Open Mic ni kuwakuza wasanii wadogo ili kufikia malengo yao na kuwa wasanii wakubwa na kupewa misingi mizuri ya kuwa wasani bora katika fani ya kuimba kama walivyo wasanii wengine.

Aliongeza kuwa kama kama wewe ni msanii na una ndoto ya kuja kuwa msanii mkubwaaa bhasi hakuna sehemu nyingine inayoweza kukupa nafasi kirahisi kama Epic Open Mic.
kama wewe ni msanii na una ndoto ya kuja kuwa msanii mkubwaaa … EPIC OPEN MIC inakuhusuuu”.

Wakali hao wa Bongo wanaotamba na ngoma zao kibao wataanza kukisanua mida ya saa nane mchana mpaka time ile ya kumi na mbili za jioni huku wasanii wadogo wenye lengo la kuwa kama wao wakishuhudia nini kaka zao wakifanya na ikifika wakati wao nao watapewa nafasi ya kufanya yao pia.









0 comments:

Post a Comment