Wednesday, May 8, 2013

MAIMATHA AFUNGUKA JUU YA MANYELE KIGORI


Shindano la kunengua la Manywele Kigori wa Extra Bongo sasa limefika patamu mazoezi yanatarajiwa kuanza mwisho wa mwezi huu.

Maimatha Jesse ambae ni mwaandaaji wa tamasha hilo amesema kuwa atakutana na waandishi wa habari wiki ijayo kutoa ufafanuzi zaidi kuhusiana na shindano hilo ambalo miaka ya nyuma lilikuwa likijulikana kama 'Manywele Kimwana wa Twanga Pepeta'

"Nitakutana na waandishi wa habari ili kuwaelezea kwa undani zaidi, lakini mwishoni mwa mwezi huu tutafanya uzinduzi wa shindano letu na kisha vigori wataanza rasmi mazoezi,"

Alifafanua kuwa uzinduzi wa mazoezi ya vigori utashirikisha wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya na kwamba wakati wa mazoezi washiriki watakuwa wanajifunza kucheza mitindo mbalimbali ya bendi ya Extra Bongo.

"Ndiyo maana shindano likaitwa Manywele Kigori wa Extra Bongo, hivyo wakati wa fainali vigori watachuana kwa kucheza mitindo mbalimbali ya bendi hiyo ambayo kwa sasa inaonekana kuwa juu kuliko nyingine.

0 comments:

Post a Comment