Wednesday, May 8, 2013

LWAKATARE AFUTIWA MASHTAKA YA UGAIDI



Mahakama kuu ya kanda ya Dar es salaam leo imemfutia mashtaka ya Ugaidi aliyokuwa nayo  Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na maendeleo Bw Wilfred Lwakatare.

Taarifa kutoka Mahakamani zinasema kuwa Lwakatare amebakiza shitaka moja la Utekaji ambalo pia linanafasi ya Dhamani 

Lwakatare alikamatwa na jeshi la polisi na kufikishwa mahakamani na kushatakiwa kwa kesi ya Ugaidi na Utekaji baada ya kuvuja kwa Video iliyokuwa akionesha kuwa Mkurugenzi huyo alishiriki katika kupanga njama za kigaidi na kuwashambulia baadhi ya watu wakiwamo waandishi wa habari nchini.

Kutokana na mashtaka  yaliyokuwa yakimkabili Lwakatare hakuweza kupata mdhamana .

0 comments:

Post a Comment