Monday, May 6, 2013

KAULI YA JANUARI MAKAMBA DHIDI YA RUGE/WANANCHI


Mbunge wa Jimbo la bumburi na Naibu Waziri wizara ya mawasiliano nchini Mh Januari Makamba ametoa kauli yake dhidi ya vita ya kimuziki iendeleayo kati ya Viongozi wa Clouds media na msanii wa muziki Lady jaydee.

kauli hiyo ameitoa kupitia ukurasa wake wa Facebook leo baada ya kiongozi mmoja muandamizi wa Radio hiyo kutumia muda mwingi kuzungumzia suala la kupigwa kwa nyimbo au kutopigwa kwa nyimbo katika vituo vya Redio mbalimbali,Mh Makamba alilifananisha suala hilo ni sawa na kukosa uzalendo katika taifa kama tanzania linalo kabiliwa na matatizo mengi ya msingi na yenye kuihitaji kutatuliwa na kutafutiwa ufumbuzi.

Kama Taifa tunayo matatizo makubwa zaidi ya kujadili na kutafuta ufumbuzi zaidi ya kutumia muda mwingi kujadili ni nyimbo za nani zinapigwa kwenye redio stesheni hii au ile na za nani hazipigwi”

MTIZAMO WANGU KWA KAULI YA RUGE “MSIPIGE BONGO FLEVA”

katika Mazungumzo aliyoyafanya Kiongozi wa Redio ya Clouds Fm Ruge Mutahaba katika kipindi cha Power Breakfast alimaliza kwa kutoa amri kwa wafanyakazi wa Redio hiyo kutocheza muziki wa bongo Fleva siku ya leo na amefanya hivyo kuonesha nguvu yake kama Ruge kuwa anaweza kufanya chochote na wakati wowote katika Redio hiyo hivyo kwangu mimi naona kweli si mahitaji ya watu kusikiliza kile alichoamrisha boss huyo.

Nikuache na swali kidogo KWA KAULI HIYO CLOUDS FM NI REDIO YA WATU​?

NA je kama wasanii wa bongo fleva nao wakiweka mgomo kwa nyimbo zao kutochezwa katika kituo hicho nini kitatokea?

Muda mwingine Busara ndiyo jibu kwa matatizo.

0 comments:

Post a Comment