Monday, May 6, 2013

MWANAMKE APORWA NA KUULIWA NA MAJAMBAZI DAR


Watu wanao sadikiwa kuwa ni majambazi wameua na kupora fedha taslimu zaidi ya millioni kumi jijini dar es salaam.

Tukio hilo limetokea mchana wa leo jijini dar es salaam baada ya wati hao kumpiga risasi mwanamke mmoja ambae jina lake halijafahamika kwa haraka na kusababisha kifo chake hapo hapo na kupora fedha zaidi ya milioni kumi.

Kwa mujibu wa chanzo kisicho rasmi kilisema kuwa mwanamke huyo alikuwa ametoka katika Bank ya CRDB tawi la Uhuru na kuvamiwa na majambazi hao waliokuwa wakitumia usafiri wa bodaboda baada ya kuligonga gari alilokuwa akilitumia dada huyo,alipotoka nje ya gari ili kujionea namna gari lake lilivyohalibika ndipo walipompiga risasi na kupora pesa hizo na kutoweka kusiko julikana.

Mwanamke huyo amepigwa risasi kifuani na kusababisha kifo chako hapo hapo.

0 comments:

Post a Comment