Tuesday, May 7, 2013

CHUO KIKUU CHA KAMPALA INTERNATIONAL CHASIMAMISHWA KUTOA MAFUNZO



Chuo kikuu cha kampala University KIU kilichopo jijini Dar es salaam maeneo ya Gongolamboto kimesimamishwa kutoa mafunzo ya Shahada za Uzamili na Uzamivu kufuatia kukuendesha mafunzo kinyume na Utaratibu na kutokuwa na wahadhiri wakutosha na wenye sifa.

Tume ya Vyuo vikuu TCU katika mkutano wake wa hivi karibuni ulikiamuru Kampala International University, Kampasi ya Dar-es-Salaam yafuatayo;

  1. KIU isimamishe mara moja mafunzo yote ya shahada za juu (Postgraduate) ikuwa ni pamoja na Shahada za Uzamili (Masters) na Shahada za Uzamivu (PhD) katika kampasi ya Dar-es-Salaam
  1. KIU ishirikiane na wanafunzi wote iliyowadahili katika programu zilizotajwa hapo juu waweze kuhamia kwenye vyuo vingine vyenye idhibati ya kutoa mafunzo hayo.

Tume haitatambua shahada yeyote ya Uzamiili au Uzamivu itakayotolewa na chuo hicho kwa watakaosoma katika kampasi ya Dar-es-Salaam.

Angalizo:
Chuo cha KIU Kampasi ya Dar-es-Salaam kina ithibati na kitaendelea kutoa mafunzo ya shahada ya kwanza (Bachelors), Diploma au vyeti
zilizopitishwa na TCU kwa mujibu wa Ithibati ya Chuo Husika.

Imetolewa na:
Katibu Mtendaji
TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA (TCU)

0 comments:

Post a Comment