Tuesday, March 12, 2013

MAKADINALI WAKUTANA ROMA KUMCHAGUA PAPA


Mwandishi kitalima gerald/kwa msaada wa mtandao

Zaidi ya makadinali mia moja wamekutana Roma ITALIA leo kwa ajiri ya kumchangua PAPA atakae liongoza kanisa katoliki Duniani kama kiongozi wa kiroho kwa wakristu Duniani kote.
 Makadinali 115 walihudhuria misa maalumu iliyofanyika katika kanisa la St Peter’s Basilica mjini Roma Italia.
Mchana huu makadinali hao wataendelea na mchakato wa kumchagua Kiongozi mpya wa wakristu Duniani kote kitendo ambacho kitafanyika kwa siri kubwa.
Makadinali hao watachagua kwa mara nne kila siku mpaka Robo tatu ya makadinali watapokubaliana na jina husika la kiongozi alioteuliwa au kuchaguliwa.
Uchaguzi huu umefuatiwa kujiudhuru kwa Benedict xvi mwezi uliopita baada ya kujiona anahitaji kupumzika kufuatia umri wake kuwa mkubwa,Hivyo kushindwa kuongoza,mpaka anajiudhulu Benedict xvi alikuwa na umri wa miaka 85.






0 comments:

Post a Comment