Tuesday, March 12, 2013

KIKOSI CHA TAIFA STARS KUIVAA MOROCCO KUTAJWA KESHO


 Mwandishi Gerald Kitalima
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Kim Poulsen kesho Machi 13 atataja kikosi kitakacho shikana shati na timu ya Morroco katika mchezo utakao chezwa katika viwanja Kiwanja cha Taifa March 24 mwaka huu Dar es salaam.

Kim poulsen atakutana na waandishi wa Habari katika mkutano utakaofanyika katika ofisi za shirikisho la mpira wa miguu Tanzania maeneo ya Karume kesho mida ya saa tano asubuhi.

Kutokana na kuendelea kwa ligi ya vodacom bara na wachezaji wengi kuonekana kufanya vizuri kesho ndipo tutajua mchezaji yupi alifanya vizuri zaidi mpaka kuonekana na kupendekezwa kuingia katika kikosi cha taifa kinachoongozwa na kocha paulsen.



0 comments:

Post a Comment