Hata
hivyo, Logarusic amesema hajakata tamaa hadi mechi ya mwisho ya msimu
kwa sababu atakutana na mabingwa watetezi, Yanga Aprili 27, mwaka
huu.
Logarusic
alisema sare aliyoipata juzi, Jumamosi dhidi ya Mbeya City imezidi
kupoteza matumaini yao ya kuivua Yanga ubingwa msimu huu.
Alisema
matokeo hayo mabaya kwa Simba yanatokana na kikosi chake kuwa na
baadhi ya wachezaji wasiostahili kuichezea timu hiyo iliyowahi
kucheza fainali za Kombe la Shirikisho barani Afrika 1993.
"Niko
katika wakati mgumu, ila kuna wachezaji wanaipa timu matokeo mabaya
kutokana na kuwa na viwango vya kati vya kuzichezea timu nyingine na
si Simba," alisema Logarusic.
Kocha
huyo alisema endapo Yanga, Azam na Mbeya City zitafanya vibaya ndiyo
Simba itarudi katika harakati za kusaka tiketi ya kushiriki
mashindano ya kimataifa mwakani.
0 comments:
Post a Comment