Wednesday, October 23, 2013

VIJANA WAFUNGWA MIAKA 120 KWA KUTEKA GARI LILIROBEBA MAITI

Vijana Wanne wamehukumiwa katika Mahakama ya Wilaya Singida  kutumikia vifungo vya miaka 120 jela kwa kuteka gari
lililokuwa likisafirisha maiti kutoka mkoani Morogoro kwenda Musoma mkoani Mara na kupora waombolezaji kompyuta na fedha.

Waliohukumiwa vifungo hivyo kila mmoja miaka 30 jela ni Hamis Ali (23), Hamisi Issa (33);  Khaldi Hamis (21) na Abubakari Jumanne (26), wakazi wa Kisaki Manispaa ya Singida.

Mshtakiwa wa kwanza Iddi Omari (38), aliachiwa huru baada ya mahakama hiyo kukosa  ushahidi wa kumtia hatiani. Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Flora Ndale, alisema ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka bila kuacha shaka umethibitisha washtakiwa hao walitenda kosa hilo.

0 comments:

Post a Comment