Na Gerald Kitalima
Msanii Omary Nyembo
alimaarufu kama Ommy Dimpoz amefunguka na kusema kuwa watu wa
uhamiaji
duniani kote huwa hawatambui umaarufu wa mtu pindi
wanapogundua kuna kitu hakijaenda sawa,Ommy Dimpoz amefunguka hayo
leo kapitia ukurasa wake wa Intrgram baada ya mwimbaji kutoka
Marekani Chris Brown kuzuiliwa kuingia Canada na kusababisha
kusitishwa kwa show zake mbili ambazo alitakiwa kuzifanya Canada
ndani ya wiki hii.
Ommy Dimpoz ameonyesha njisi
gani watanzania na mashabiki wake walilipokelea suala lake tofauti na
kuonyesha kuwa watu wengi walimcheka na kumchamba wakiamini kuwa yeye
ni mtu maarufu hivyo asingeweza kupatwa na suala hilo.
"Pole braza
Kristofa,haya ni Mambo ya kawaida ila Mwenzio nilivyozuiwa kuingia
Nchini kwenu Basi nilivyorudi kwetu nimechekwaaa,Nimechambwaa
khaa,hawajuagi mambo ya Uhamiaji hawajali we nani."
Wiki kadhaa zilizopita msanii
Ommy Dimpoz alirudishwa Tanzania baada ya kuzuiwa kuingia Marekani
kwa kukosa vibali vinavyomruhusu kuingia nchi hiyo kufanya show.
0 comments:
Post a Comment