Na Gerald Kitalima
Msanii ambae pia ni kiongozi
wa kundi la East Coast Team GK amesema sasa ni wakati sahihi kwake
kurudi
katika muziki na kufanya kazi ya muziki baada ya kumalizana na
masuala ya shule,GK ambae anatarajia kuachia kazi yake
mpya siku ya
Jumatatu ambayo amemshirikisha msanii Vanessa Mdee na kazi hiyo
imetayarishwa na produza mkongwe John Mahundi na Markochali.
King Crazy GK alidai kuwa
John Mahundi ilibidi asafiri kutoka Marekani na kuja bongo kufanya
kazi hiyo ambayo anaamini watanzania watampokea na kumuelewa baada ya
kimya cha muda mrefu,Mkali huyo mwenye miondoko ya michano amedai
kuwa kazi hiyo ambayo itatoka siku ya Jumatatu imesimamiwa na msanii
Ay.
"Kama unavyotuona hapa
mapishi yameshakamilika na watanzania wakae tayari kwa kazi nzuri
kutoka kwangu nikiwa na Vanessa Mdee,naamini mashabiki zangu
wananisubiri na mimi nasema kwa sasa siwezi kuwaangusha kabisa,maana
kama masomo yamekwisha kwa sasa ni kazi tu na wategemee mambo mengi
kutoka kwangu na kutoka kwa East Coast Team nzima"
Msanii King Crazy GK kwa mara
ya mwisho alitoa wimbo wake wa mwisho uliokuwa na maadhi ya Kwaito
ambao alifanya na Yuzo na wimbo huo ulifahamika kama Baraka au laana?
ambao haukufanya vizuri sana katika vyombo mbalimbali vya habari.
0 comments:
Post a Comment