Na Gerald Kitalima
Msanii Dogo Janja ambae kwa sasa amerudi chini ya
uongozi wake wa zamani amefunguka ya moyoni na kusema kuwa katika
kipindi
kirefu watu wamekuwa wakimzungumzia vibaya na kumsema kuwa
amepotea katika muziki wa Bongo,Dogo Janja amefunguka hayo leo baada
ya jana kuweza kufanya show kali katika viwanja vya Mwananyamala na
kupokewa vizuri na mashabiki wake ambao walionyesha kumkubali
Janjaro.
"Wapo Waliosema Janja Aliotea/Janja
Kapotea/Janja Ameanguka HaweZi Simama Akatembea/ Mtaani Maneno
Kibao,Mpaka kwenye Mitandao ya kijamii Watu Wanakusema Utadhani
Unakula Kwao..!Hii ilikua Jana Viwanja Vya Mwananyamala Uzinduzi
Wa............ Mungu Akubariki Father Madee Ali Mungu Akutie Nguvu
Tuzidi Kusonga NP: Janjaro Bado Yupo Kama Desturi Na Mila."
Mwanamuziki Madee Ali kutoka Tip Top Connection siku
za karibuni alipokuwa katika kipindi cha The Cruise ya East Africa
Radio alisema kuwa wakati wa Dogo janja kurudi katika game umefika na
muda wowote kuanzia sasa ataachia wimbo wake mpya ambao nao
ushakamilika.
Dogo Janja alikuwa chini ya usimamizi wa Madee kabla
ya kushindwana na kutimukia katika kundi la Mtanashati Entertainment
lililokuwa chini ya uongozi wa Ostadhi Juma na Musoma lakini hata
hivyo kundi hilo liliweza kutamba kwa muda na kupotea huku Dogo Janja
nyota yake ikionekana kupotea ndipo alipoona haja ya kurudi kwa baba
yake mlezi ambae alimfunza muziki na kumsimamia katika maisha ya kila
siku Madee Ali.
0 comments:
Post a Comment