Na Gerald Kitalima
Msanii nguli wa bongo Fleva Judith Wambura maarufu
kama Lady Jaydee amefunguka na kuweka wazi kuwa katika maisha yake ya
kawaida,maisha ya sanaa na maisha ya utafutaji amekuwa akikutana na
changamoto mbalimbali zinazopelekea muda mwingine mpka watu kugombana
au kutofautiana kutokana na mtazamo au matatizo mbalimbali na amedai
wazi kuwa katika watu wote ambao aligombana nao na yeye kugundua
ndiye alikuwa chanzo cha ugomvi huo wote alishawaomba msamaha na
wanaendelea na maisha ya kila siku.Lady Jaydee alisema hayo jana
kupitia ukurasa wake wa Instragram wakatia akijibu maswali 10
yaliyotokana na maswali kibao kutoka kwa mashabiki wake.
"Nitapatana na mtu atakae kubali kuwa alikosa,
km naamini yeye ndio alinikosea itabidi aniombe msamaha.Kama mimi
ndio nilikosa nitaomba pia msamaha Otherwise hakuna miujiza Siwezi
kumuomba mtu msamaha endapo naamini kabisa sijakosa .Niliowahi
kuwakosea nilishawaomba msamaha wooote.Hakuna binadamu asie kosea ila
siwezi ku surrender kiuongo au kwa uoga wa maisha.Naamini hata
nikiuza nyanya bado wapo watu wanaohitaji nyanya, na watanunua."
baadhi ya mashabiki waliuliza kwanini Lady Jaydee
hana ushirikiano na wasanii wenzake wa kike katika muziki na yeye
aliweka wazi kuwa amekuwa akishirikiana nao sana tu mpaka kufikia
hatua wengine kuwatungia wimbo,Jide anadai kuwa mara nyingi ili
msanii aweze kutoka au kufanya vizuri lazima kazi zake zipate promo
ya kutosha katika vituo mbalimbali vya Redio na bahati mbaya yeye sio
mwenye hizo redio.
Nimewahi kufanya na wasanii mbali mbali wa kike ila
sijui kwanini hamjaziskia.
1.Mwasiti amewahi kunishirikiisha
2. Nimewahi kumuandikia na kushiriki kuimba kwenye
wimbo wa movements za Albino na Kaysha
3. Nimewahi kumwandikia na kushiriki kuimba nae
Nakaaya Sumari
4. Nimewahi kumwandikia wimbo Patricia Hillary
5. Nimewahi kumshirikisha RAY C kwenye wimbo wangu
toka Album ya Machozi unaitwa, Nimekubali na wapo wasichana mbali
mbali waliopita Machozi Band na kujifunza kuimba leo
mnawafahamu,Kumbukeni tu kuwa kutoka kwa mtu itategemea na nyimbo
zake kuwa promoted redioni na mimi sio mwenye hizo redio.Msaada pekee
ni kushiriki kila ntakapotakiwa kufanya hivyo"
Lady Jaydee kwa sasa anatamba na wimbo wake wa
Forever ambao amemshirikisha mdogo wake anaefahamika kama Dabo na pia
mwanadada huyo amepanga kufunguka mengine mengi ambayo nayo
tutakuletea kupitia www.eatv.tv
0 comments:
Post a Comment