Monday, February 17, 2014

TUZO ZA KILIMANJARO MUSIC AWARDS 2014 KUZINDULIWA LEO

Waandaaji wa Tuzo za Kilimanjaro Music Awards kampuni ya bia ya Kilimanjaro leo inazindua rasmi mchakato wa kuwapata wakali waliofanya vyema katika tasnia
ya muziki kwa mwaka 2013.

Kampuni ya bia ya Kilimnajaro kupitia ukurasa wake wa Face-book na Twitter wameweka wazi kuwa tuzo hizo zinazinduliwa leo na kutoa nafasi kwa mara ya wapenzi wa muziki kupendekeza wasanii watakaoingia kwenye kinyang'anyiro hicho kwa mwaka huu.

Tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2014 zinazinduliwa rasmi siku ya leo. Kwa mara ya kwanza katika tuzo za #KTMA2014 wapenzi wa muziki watapewa nafasi ya kupendekeza wasanii watakaoingia kwenye kinyang'anyiro.”

Kwa kusisitiza hilo washabiki wataweza kuchangia mapendekezo yao juu ya aina gani ya wasanii wanapaswa kushiriki zoezi hilo kupitia tovuti na njia ya SMS.

0 comments:

Post a Comment