VIGOGO
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwemo wabunge, wamemjia juu Mkuu wa
Mkoa (RC) wa Arusha, Magessa Mulongo kwa jinsi alivyoshughulikia kesi
ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA).
Wabunge
hao waliliambia gazeti hili mjini Dodoma kuwa kesi ya uchochezi
iliyofunguliwa na serikali dhidi ya Lema kwa shinikizo la mkuu huyo,
itaiathiri kwa kiasi kikubwa CCM.
Mbunge
wa Mwibara, Kangi Lugola alisema kuwa amefuatilia kwa makini chanzo
cha kesi ya Lema na hatimaye kukamatwa na polisi mithili ya gaidi, na
kubaini kuwa hulka za utendaji kazi wa baadhi ya viongozi wa serikali
zinawapa sifa na umaarufu zaidi CHADEMA.
“Mimi
sitaki kuingilia kesi, lakini ukiangalia kuanzia ile inayoitwa video
ya vurugu za Chuo cha Uhasibu Arusha na jinsi Mkuu wa Mkoa alivyofika
eneo la tukio na kuondoka, utabaini udhaifu mkubwa wa kiongozi huyo
ambao leo unamfanya Lema aonekane shujaa.
“Leo
tunaingia kwenye uchaguzi mdogo wa madiwani pale Arusha, tunaweza
tukashinda, lakini tutafanya kazi ya ziada kwa sababu tu ya udhaifu
wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha,” alisema Lugola.
Mbunge
mwingine ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe, alisema alichokifanya
Mulongo ni sehemu ya tatizo kubwa la viongozi wa serikali kujihusisha
na ukereketwa wa kisiasa.
“Baba
wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa kuna kiongozi, tena
hakumtaja jina, kwamba anapendwa kubebwa, alisema mwacheni abebwe.
Alisema vile kuwazuia polisi kukabiliana na watu wanaopenda kumbeba
kiongozi huyo.
“Mkuu
wa Mkoa Arusha na wengine wanaokabiliana na wapinzani kwa nguvu kubwa
bila sababu, hii inawaongezea umaarufu,” alisema mbunge huyo kutoka
moja ya majimbo ya kanda ya kati.
SOURCE CHADEMA BLOG
0 comments:
Post a Comment