Thursday, May 2, 2013

MSIGWA ATEMA CHECHE BUNGENI JUU YA MGOGORO WA LOLIONDO



Akizungumzia mgogoro wa ardhi wa Loliondo Waziri kivuli wa wizara ya maliasili na utarii mchungaji msingwa amesema kuwa Mgogoro huo wa Loliondo umejengwa na serikali iliyopo madarakani hivyo serikali haina nia ya kutatua mgogoro huo.

Msigwa amesema kuwa tunapozungumza masuala ya masirahi ya taifa ni bora kuachana na siasa zisizo na maana kwani wote wapo katika boti moja hivyo busara ichukuliwe na mawazo ya watu wa pande zote wanahusika.

Msigwa amesema kuwa serikali ya Chama cha mapinduzi inahusika moja kwa moja na masuala ya ujangiri kutokana na kuwa na mtandao mkubwa wa viongozi wanao hujumu mariasili ya taifa letu la Tanzania.

Serikali inahusika moja kwa moja katika ujangiri na migogoro ya ardhi iliyopo ndio maana serikali ya chama cha mapinduzi na viongozi wake hawana kauli yoyote ile juu ya masuala hayo.

0 comments:

Post a Comment