Sunday, December 22, 2013

IVO AMSHANGAA JUMA KASEJA

Kipa wa Simba Ivo Mapunda Ameshangazwa na Kipa Mwenzake wa Yanga Juma K Juma kutokana na Kipa huyo wa Yanga kutompa mkono wa salamu walipokuwa
Uwanjani mbele ya Wageni Rasmi.

Kabla ya kuanza kwa mchezo huo uliomalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-1, Kaseja aligoma kumpa mkono Ivo wakati wachezaji wa timu zote mbili wakisalimiana mbele ya Mgeni Rasmi wa mchezo huo, Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe ambaye alikuwa amefuatana na Rais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jamali Malinzi na Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, George Kavishe.

"Soka ni sehemu nzuri ya kukutanisha watu, nimekutana na Kaseja uwanjani na nilitegemea atanipokea vizuri kama Mtanzania na mchezaji mwenzake, lakini amenishangaza sana kwa kuninyima mkono," alisema Ivo.

"Sijawahi kutukanana wala kuwa na mgogoro wowote na Kaseja.

Alichokifanya ni picha mbaya kwa wapenzi wa soka, hasa watoto ambao wanatuangalia sisi (wachezaji) kama kioo chao,"

0 comments:

Post a Comment