Wednesday, May 1, 2013

AY ADONDOSHA NGOMA MPYA IJUMAA HII



Msanii maarufu kutoka Tanzania anaefanya vizuri katika Tasnia ya muziki wa bongo Fleva Nchini na Nje ya mipaka ya Tanzania Ambwene Yesaya alimaarufu kama AY.

AY anatarajia kuachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la JIPE SHAVU aliompa shavu msanii Fid Q kutoka pande za Rock City Mwanza vilevile wimbo huo umetengenezwa katika studio Mpya itwayo Mpo Afrika chini ya Producer Q.

Ijumaa naachia wimbo wangu mpya huo nilioufanya na Fid Q baada ya kukamilika hivyo mashabiki wakae tayari kwa wimbo huop ijumaa hii”alisema AY

AY anatarajia kuachia wimbo wake lakini mwezi uliopita msanii huyo alishirikiana na Mwanafalsafa MWANA FA pamoja na J Martin kutoka Nigeria na kutengeneza wimbo waliosema ungetoka mwishoni wa mwezi wa nne au mwanzoni wa mwezi huu wa tano baada ya kufanya Kichupa cha Wimbo huo. 

0 comments:

Post a Comment