Thursday, May 23, 2013

ROMA -WATANZANIA WANATAKA MABADILIKO



Msanii wa Hip Hop Roma Mkatoliki anaetamba na ngoma yake ya 2030 alieifanya maalumu kwa ajiri ya mwanae na watanzania kiujumla amefunguka kuwa watanzania sasa wanahitaji mabadiliko na kama hawawezi kuyapata mabadiliko ndani ya chama tawala basi watayafuata mabadiliko nje ya Chama hicho.

Watanzania wanataka mabadiliko/ wasipoyaona na wasipoyapata ndani ya ccm watayatafuta nje ya ccm!Kiongozi bora hawezi toka nje ya ccm”

Mkali huyo wa miondoko ya Hip Hop mwaka jana katika tuzo za KTM ametiririka hayo siku moja baada ya wananchi wa Mtwara kufanya fujo na vurugu zilizosababisha watu kadhaa kupoteza maisha yao huku wengine wengi wakijeruhiwa kutokana na vurugu hizo na kusababisha uhalibifu wa mali za watu ikiwa ni pamoja na kuchomwa kwa nyumba za viongozi,kuvunjwa kwa daraja yote ni katika kupingana na kauli ya serikali juu ya kutaka kusafirisha Gas kutoka Mtwara na kuipeleka Dar es salaam.




0 comments:

Post a Comment