Saturday, January 19, 2013

SHILOLE WASANII WA FILAMU MAJUNGU TU





MCHEZA sinema na muimbaji wa bongo fleva anaemiliki kampuni ya Shilole Classic amefunguka na kusema kuwa wasanii wa filamu wametawaliwa na majungu na kutokuwa na upendo wa kweli kati yao hali ambayo huwafanya kutokuendelea kwani muda mwingi huutumia kufuatilia maisha ya watu. 

Shilole alifunguka maneno hayo alipokutana katika one to one interview na Mpita njia katika Hoteli ya Lamadar jijini Dar es salaam alisema kuwa wasanii wa bongo fleva wamekuwa na upendo kati yao na wanashirikiana katika mambo mbalimbali hata nje ya kazi zao lakini si kwenye tasnia ya Filamu. 
SHILOLE

Aliendelea kutiririka kuwa katika mwaka wa jana kutokana na ushirikiano mzuri alioupata kwa wasanii wa bongo fleva umemsaidia yeye kufanya show nyingi mno kwa wasanii wa kike Tanzania hayo mafanikio yamekuja kutokana na ushirikiano mzuri alioupata kutoka kwa wasanii wa bongo fleva.

0 comments:

Post a Comment