Saturday, January 19, 2013

WASANII WACHANGA NJOONI DAR LIVE




Na Kitalima Gerald 

WASANII wachanga wa Filamu wameombwa kujitokeza kwa wingi katika Tamasha la Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) litakalo fanyika siku ya Jumamosi ya Tarehe 26 katika Uwanja wa Taifa wa Burudani Dar Live.

Wito huo ulitolewa na Rais wa Shirikisho la Filamu Simon Mwakifwamba alipokuwa akieleza lengo la tamasha hilo.”wasanii wachanga wajitokeze kwa wingi siku ya tamasha kwani ndio sehemu yao kuonesha vipaji vyao siku hiyo kutakuwa na wasanii mbalimbali hivyo wanaweza pata fursa ya kuonekana na wakapewa nafasi na wakongwe katika kazi zao”
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Simoni Mwakifwamba

Akizungumzia wasanii wa filamu watakao fanya show katika muziki ni pamoja na Shilole,Sunura,Joti,Masanja Mkandamizaji,Hemedi ‘PHD’,Kitale lakini Twanga pepeta,Tundaman pia watafanya show kali siku ya Jumamosi.

0 comments:

Post a Comment