Saturday, January 19, 2013

HAKUNA SUPER STAR BILA SHABIKI-SUNURA




Na Kitalima Gerald 

MUIMBAJI na mcheza sinema za bongo Snura Mushi mtoto wa kibosho anaetamba na kibao cha majanga amefunguka na kusema hakuna star bila shabiki.

Snura amefunguka hayo pale alipokuwa akiwaomba watanzania wajitokeze kwa wingi katika tamasha lililoandaliwa na Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF)litakalofanyika katika ukumbi wa Dar Live siku ya Jumamosi ya tarehe 26

“Nawaomba watanzania wajitokeze kwa wingi waje kupata raha na kubadilishana mawazo na wasanii mbali mbali nikiwemo mama yao Snura,Shilole,Joti,Hemedi,Masanja mkandamizaji,Twanga pepeta maana hakuna super star bila shabiki hivyo watokeze kwa wingi kutuenzi na kutufaliji”
SNURA MUSHI

Onesho hilo limeandaliwa na Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) likiwa na lengo la kukutanisha wadau mbalimbali ambao watalisaidia shirikisho la filamu Tanzania kuweza kupata vifaa vya ofisi na kupata ofisi inayoendana na hadhi ya shirikisho.

0 comments:

Post a Comment