Saturday, January 19, 2013

RICHARD MAVOKO NINGECHEZEA SIMBA




Na Kitalima Gerald 

MKALI wa bongo flava Richard Mavoko anaetamba na ngoma kama mary me,silali na One time amefunguka na kusema asingeweza kufanya vizuri katika muziki wa bongo fleva angekuwa mchezaji wa msimbazi.
MAVOKO

Mavoko aliendelea kutiririsha ukweli huo kwamba kabla ya kufanya muziki alikuwa mchezaji mzuri wa soka na alikuwa akichezea namba 9 na katika soka alifahamika kwa jina la ‘Etoo’ kutokana na uwezo wake wa kufumania nyavu za wapinzani wake kila alipocheza mechi.

“Kweli kabsa walikuwa wakiniitaEtoo kwani ukicheza na mimi ni lazima nikufunge utake usitake haijawahi kutokea nicheze mechi halafu nisishinde,nilishaanza kufanyiwa mpango wa kwenda kucheza soka Simba FC  hivyo kipaji cha soka kipo na kama muziki ungenishinda ningesakata 
kabumbu na watanzania wangenielewa tu” 

Pindi alipoulizwa ni kwanini angecheza Simba na si Yanga alidai kuwa yeye ni mnazi wa Msimbazi  hivyo angecheza Simba kwakuwa  na mapenzi na Club hiyo na ndoto ya kucheza soka ilikufa pale alipoweza kufanya vizuri katika muziki wa bongo flava.
RICHARD MAVOKO
RICHARD MAVOKO


 Akizungumzia  ngoma yake mpya One Time ambayo amefanya chini ya C9 amesema wimbo huo amemzungumzia mwanaume ambae anampango wa kuongea na msichana asie na wazo na huyo mwanaume,”video ya one time inafanywa na Adam Juma wa Visual Lab hivyo muda si mrefu itakuwa tayari luningani”Mavoko alisema.

0 comments:

Post a Comment