Na Gerald Kitalima
Mwanamuziki nguli wa kike
hapa Tanzania Lady Jaydee ambae kwa sasa anafanya poa na wimbo wake
wa Forever amefunguka na kuonyesha kukerwa na kitendo cha
baadhi ya
mashabiki wake wa Instgram ambao walimuelewa vibaya baada ya kupost
picha jana na kusema kuwa tumbo lake limevimba baada ya kupata msosi
wa maana na mzuri,Mashabiki hao wengi wao walitafsiri kuwa Mwanadada
huyo kwa sasa ni Mjamzito baada ya kuona picha ile na maneno ya Jide
yaliyosomeka kama Tumbo limevimba sababu ya sahani.
Lady Jaydee alibidi aifute
ile post aliyopost na kupokelewa tofauti na baadhi ya mashabiki wake
na kisha aliandika maneno haya kuonyesha kutopendezwa kabisaa na
baadhi ya mashabiki walioshadadia kuwa ametundikwa mimba,huku wengine
wakionyesha kumnyanyapa.
"Imebidi nifute post Ili
nielezee upya.Hivi watu hamuelewi kiswahili au ni nini ??? Nimesema
tumbo limevimba sababu ya sahani,nikimaanisha mlo na nili post nakula
hapo awali Sasa hayo maneno mengine yanatokea wapi? Au niwe naandika
kichina? Kwani mliambiwa nitazaa Rais atakaewatoa ktk shida zote mpka
mnishikilie mimba mimba
Hebu niacheni basi khaaa
Nisiishi Kisa mimba? Aisee mnaboa sana.Basi niueni Kisa sijazaa Ili
niwaondolee kero kabisa."
Mashabiki wa Lady Jaydee
wameonyesha kumtia moyo mwanadada huyo baada ya mashabiki wengine
kuanza kuandika vitu vibaya huku wengine wakimzihaki kuwa hawezi
kupata ujauzito na kumwita majina ya ajabu ajabu mwanamuziki huyo.
"Mwangaza84: Fanya yako
mama, binadamu hawakosi la kuongea.Kwani mtu bila mimba maisha
hayaendi? Stupid pipo always think about t stupid things.youre the
best and you do best music ever in Tanzania hatotokea kama wewe. Big
up sisister"
"Ilotha_boniphace: "Hayo
nimapenzi ya mungu namungu ndio amepanga usijali Jide huyu huyu mungu
alie kupa uhai ndo atakupa haja yamoyo wako nahayo nimaneno ya
binadamu yanapita but ya mungu kamwe hayapiti so jipe moyo my sister"
"Martha_mollel: Hata wao
wanavizazi kama wanataka watoto wakazae wao, wakuache, binadam bwana
mnaboa mimba mimba si mzae na nyie, mafi yenu..."
"Jokofu2: Kila kitu ni
majaliwa ya allah kuongelea jambo usilolijua nimpango wa kibinadamu,
hivo puuza na usiumize kichwa dada jide."
0 comments:
Post a Comment