Na Gerald Kitalima
Rama Dee amefunguka hayo
kupitia ukurasa wake wa Facebook alipodai kuwa mashabiki na upungufu
wa muziki wa RnB Tanzania ndicho kilichomsukuma
kufanya kazi hiyo.
"Kikubwa nilichokifanya
kwenye hii nyimbo mpya ya USIHOFIE WACHAGA, Ni hasira za mapungufu ya
ladha za RnB zilizokuwa chini hapa Nyumbani.Bado najifunza mengi na
kufunza wengi pia.Fans wangu wananipa hasira sana,na nitazidi kufanya
kwa faida yenu siku zote."
Kazi mpya ya Rama dee
imetengenezwa na ELY DA BWAY ndie produza alie tengeneza ile ngoma
"Kama HuweZi" Mkali huyu yupo pale Ubungo (Home Town
studio) mbali na ngoma hii alitengeneza kazi mwisho ya Rama Dee akiwa
na Lady Jaydee ambayo ilitoka mwaka jana na kufanya vizuri sana
katika vituo mbalimbali.
Baada ya kuachia kazi hiyo
baadhi ya mashabiki wa Rama Dee walikuwa na haya ya kusema juu ya
kazi hiyo ambayo mpaka sasa toka imetoka inasiku tatu na kusikika
masikioni mwa watanzania walio wengi kupitia mitandao ya kijamii na
vipenid mbalimbali vya Radio.
"RJ Mkali: Mimi kwakweli
nimeisikia na nimeshaipata kupitia mitandao ya kijamii.Niseme kweli
braza we ni noma bado sijaona zaidi yako usipotee sana kaka huwa
tunakosa vitu kama hivyo"
"Erick Mlelwa: Mimi
nimeipata na nimesikiliza ila kikubwa nimegundua sauti yako ni ya
kipekee sana all in all we need your vocol all the time
"Dullahkagoda Daaah
..Wewe jamaa unajua sana RnB nasema hivi wimbo huu utaishi zaidi ya
miaka 100 ..Ama hakika upendo hauchagui kabila/humu duniani wabaya
wamewazidi wazuri Ahsante Rama Dee kwa radha ya masikio."
Kufuataia mapokezi mazuri ya
mashabiki wa Rama Dee katika wimbo huu ndio unamfanya Rama Dee kuona
bado anadeni kubwa kwa mashabiki wake ambao wanaonyesha kukosa ladha
ya muziki ambao yeye anaufanya ndio maana amesema kuwa mashabiki wake
wanazidi kumpa hasira ya kufanya kazi nzuri siku zote.
0 comments:
Post a Comment