Tuesday, April 1, 2014

KILIMO KITAWASAIDIA VIJANA-DITTO

MSANII wa muziki wa Bongo fleva ambae kwa sasa anatamba na kibao chake kipya 'Tuongeze bidii' amesema kuwa vijana wa kitanzania wajitaidi kubadili
mtazamo wao na kukiangalia kilimo kama mkombozi ,kuliko kuendelea kung'ang'ana na vitu ambavyo haviwezi kubadili maisha yao, licha ya kufanya muziki Ditto ameamua kuwekeza katika kilimo na kutegemea kilimo kubadili maisha yake kama kijana.

Ditto alisema kwa sasa anafanya muziki na amewekeza katika kilimo cha ufuta na nanasi kilimo ambacho ni cha kisasa na anategemea kunufaika na kilimo hicho kwani kabla hata ya kuanza kulima alishafanya uchunguzi wa kutosha na kugundua kuwa inawezekana ndipo alipo amua kufanya kweli.

"Ninafanya kilimo cha ufuta na nanasi ninamiliki zaidi ya ekali kumi Bagamoyo,lakini kilimo nachofanya ni kilimo cha kisasa kwani kuna vijana ambao wanasimamia na kufanya kazi na mimi nakuwa nafuatilia nini kinaendelea na kitu gani kinahitajika na kutimiza,vijana wanapaswa kufunguka na kubadili mawazo yao maana kilimo ni njia mbadala ya kujiongezea kipato na kubadili maisha yao,lakini siwezi kuwalaumu vijana maana huenda wanakosa taarifa sahihi na pia wanakosa ubunifu ndio maana wanashindwa kuziona fursa kama hizi."

Mbali na hilo msanii Lameck Ditto amewalaumu watu ambao wamefanikiwa katika maisha na hawataki kuwa mwongozo kuwashauri au kutoa siri ya mafanikio yao kwa jamii na kufananisha kitendo hicho ni sawa na ubinafsi wa kutaka maendeleo peke yako.

Wakati mwingine siwezi kuwalaumu moja kwa moja vijana kwani hata watu ambao wanafanikiwa kimaisha unapowauliza juu ya mafanikio yao wanabaki tu kukuambia komaa,wamekuwa ni wachoyo wa mawazo na wabinafsi wenye kutaka maendeleo ya kwao peke yao,ndio maana vijana wengi wanakosa taarifa muhimu ambazo zingiweze kuwasidia kufanya jambo fulani kwa maendeleo yao."

Lameck Ditto ametoa wito kwa vijana kuacha masuala ya kuigana katika biashara,sanaa au katika jambo lolote lile bali wajifunze kutafuta taarifa ambazo zitasaidia kuwa chachu katika maendeleo na kutokuogapa kufanya jambo wasichoke kujaribu na kujituma zaidi maana ndio siri kubwa ya mafanikio kwa binadamu.

0 comments:

Post a Comment