MWANAMUZIKI
na Mmiliki wa Bendi ya “Malaika music band” Christian Bella
ameamua kujitupa kufanya muzuki ambao utakuwa tofauti kidogo na iana
ya
muziki ambao amekuwa akifanya kwa miaka kadhaa,akiwa na lengo la
kuleta ladha tofauti katika muziki wake na kujiongezea mashabiki
ambao anawakosa kwa kufanya muziki wa band tu.
Christian
Bella alisema kuwa kwa sasa anaanza kutambulisha wimbo wake mpya
ambao amemshirikisha msanii Ommy Dimpoz,wimbo ambao umefanywa katika
studio za Combination Sound chini ya produza Man Walter.
Ni
kweli nimefanya aina tofauti ya muziki kwa sasa natambulisha Bongo
fleva niliyofanya na rafiki yangu Ommy Dimpoz,wimbo unaitwa 'Nani
kama mama' na nitautambulisha mwezi April mwanzoni,nitatoa Audio na
Video kwa pamoja ili mashabiki waweze kupata burudani na kupata
kumsikia na kumuona Bella akifanya Bongo Fleva"
Christian
Bella aliongeza kuwa huo ni mpango wake kwa sasa kuchanganya ladha
katika muziki wake hivyo mashabiki wakae teyari tu kwani kuna wimbo
wa RNB utafuata baada ya Nani kama mama,wimbo ambao anafikiri kufanya
na mwanamuziki wa Rnb wa hapa nyumbani huku akichanganya na msanii
mwingine wa Hip Hop.
Christian
Bella alishawahi kuwa Prezidaa wa Bendi ya Akudo Impact 'Vijana wa
Masauti' kwa miaka kadhaa kabla ya kuachana na Bendi hiyo na
kuanzisha Bendi nyingine inayofahamika kama 'Malaika music band”.







0 comments:
Post a Comment