Akizungumza
Mtayarishaji wa video ya wimbo huo Mike Tee alisema kuwa Video ya
wimbo huo ilishakamilika muda mrefu toka mwaka jana na ilipagwa
kuachiwa toka November mwaka jana lakini kuna mambo yalikuwa
hayajakamilika kiutawala kitu ambacho kimefanya mpka leo kazi hiyo
iwe bado haijatoka.
"Wimbo
ulikuwa utoke toka mwaka jana November ila aliyekuwa akisimamia ili
kazi ikamilike ametengeneza ukuta kati yangu mimi na wakuu wa jeshi,
ndio maana nimeamua kutoa wimbo huo mwezi ujao kama zawadi,ila
version yangu tofauti na kazi niliyokuwa nikifanya awali pamoja na
jeshi."
Mike
Tee alidai katika ufanyaji wa Video hiyo kulikuwa na changamoto kubwa
sana hususani katika kupata vibali kwani kulikuwa na usumbufu
sana,pia kuna sehemu ambazo hawakupewa ruksa kabisaa kushoot scene za
video hiyo lakini pia kazi walikuwa wakifanya kwa amri.
"Kwanza
ilikuwa usumbufu wa kupata vibali,kuna sehemu unaweza ukashoot
ukaambiwa hauruhusiwi ,pia upande wa malipo wamekuwa wasumbufu kifupi
kazi imeisha toka mwaka jana lakini nasumbuliwa sana,upande mwingine
wanafanya kazi kwa amri hawajui muda mzuri wa upigaji picha hivyo
imekuwa shida kidogo wakati wa ufanyaji kazi katika video hii."
Katika
wimbo huo unaokwenda kwa jina la (JWTZ) uliowakutanisha wakongwe wa
muziki Tanzania umefanywa katika Studio ya Bongo Record chini ya P
Funk majani,huku Video ya wimbo huo ikiwa imefanywa na Director Mike
Tee Mnyalu.









0 comments:
Post a Comment