Thursday, February 20, 2014

SIWASHIRIKISHI WASANII LONGOLONGO-NEY WA MITEGO

Mkali Ney wa mitego anaetamba na ngoma yake ya Nakula ujana amefunguka na kuweka wazi kuwa kazi zake kwa sasa hawezi kufanya na
wasanii ambao ni longolongo bali atafanya kazi na wasanii ambao wanatambua nini wanafanya katika muziki.

Ney amebainisha hayo alipokuwa akiweka wazi mikakati yake kwa mwaka huu 2014 ambapo amekili kuhitaji kufanya kazi na msanii Joseph Chameleone wa Uganda ambae kwa sasa amedai yupo katika hatua za mwisho za mazungumzo nae.

Mkali huyo alizidi kuweka wazi kuwa mbali na kazi hiyo anayotegemea kufanya na mkali wa uganda,anategemea kuachia wimbo mpya utakufuata baada ya nakula ujana ambayo ameshirikiana na Diamond Platnum kama ilivyokuwa katika wimbo wao wa awali muziki gani.

Ney amesema kuwa Project yake na Diamond Platnum haijaishia katika Muziki gani tu bali kuna kazi inafuata ameshirikiana nae.

0 comments:

Post a Comment