Wednesday, February 19, 2014

NYOTA YAKO LEO JUMATANO : 19/2/2014

NDOO –AQUARIUS (JAN 21 – FEBR 19)
Leo ni siku ya Bahati kwako utapata fedha au utapata faida ambayo

hukuitegemea au utasamehewa makosa ambayo uliyomfanyia mtu wako wa karibu awe mumeo, mkeo mpenzi wako au mshirika wako.

SAMAKI – PISCES (FEB 20- MACH 20)
Siku hii ya leo kuna mgeni na kitu kilichopotea ambacho unataka sana kujua habari zake.inaonekana unawaza juu ya nafsi yako,unataka kujua maisha na hali yako itakuwaje. Pana kazi au jambo ambalo unashaka nalo kama litatimia au vipi? Elewa kwamba utapata furaha kazini kwako au utaletewa biashara ambayo itakuletea faida kimaisha

PUNDA- ARIES (MACH 21- APR 20)
Leo inaonekana una hamu sana ya kukutana na mpenzi wako na kujua juu ya safari au biashara na kazi. mambo yako yataenda vizuri, Unashauriwa kuwa uwe mtulivu na hali yoyote itakayokutokea siku ya leo kwa kuwa ni hali ya muda mfupi tu.

NG’OMBE – TAURUS (APR21 – MAY 20)
Leo Haja yako itatimia. Kuna mtu mkubwa mmoja ndiye atakaye kuonea huruma kwa njia usiyoitegemea. mgonjwa wako aliye hospitali atapona au utaletewa habari ya nzuri itakayokufurahisha..

MAPACHA - GEMINI (MAY 21- JUN 21)
Unashauriwa kuwa makini na kila unachotaka kukifanya, usimamizi wa karibu unahitajika kwa kila jambo unalotaka kulifanya. Mambo yote unayotaka utayapata kwa sharti uache kuwa na wasiwasi na hofu au kupapatika, mambo yako mengi yatakwenda kwa kusuasua,

KAA - CANCER (JUN 22- JUL 22)
Leo lazima utapata kitu unachokitaka au pesa unazohitaji au mtu unayemtarajia. Mtoto au kitu kilichopotea kitarejea mambo yako mengi yatasimama, yale tu utakayoyafanya wewe mwenyewe ndiyo yatakayofanikiwa, lakini yale yote utakayoyaagiza yafanywe na watu wengine yatalala.

SIMBA - LEO (JUL 23 –AUG 22)
Jumatano ya leo ni Njema sana kwako Lazima utapata kitu unachokitaka au pesa unazohitaji au mtu unayemtarajia. Pamoja na hayo jaribu kuwa na tahadhari unaweza kupatwa na balaa la bila ya kutegemea na bila kosa lolote na hata kama lipo kosa basi kosa hilo hukulifanya wewe.

MASHUKE - VIRGO (AUG 23- SEPT 23)
Leo ni siku ambayo
,itakubidi utoe rai nzuri na uache woga na usivunjike moyo kwani patatokea upinzani na undani, kuna habari za uongo utaambiwa na Mkeo au Mpenzi wako kuhusiana na biashara zako. Jaribu kufanya uchunguzi kabla hujachukua hatua.

MIZANI - LIBRA (SEPT 24- OCT 23)
Safari unayofikiria ni nzuri, na biashara yako itafanikiwa maendeleo yako yatakuwa ni madogo na yatakuwa yanaenda polepole sana. Biashara yako pia itapanuka kwa kusuasua.

NGE - SCORPIO (OCT 24- NOV 22)
Leo ni siku nzuri kwako Mpenzi wako atarejea salama, na utashinda mitihani na adui yako atajuta Hii ni wiki nzuri ya kurekebisha makosa yote ambayo umeyafanya katika kipindi cha nyuma.

MSHALE - SAGITARIUS ( NOV 23 - DES 21)
Leo Unashauriwa kuwa kufanikiwa kwa mambo yako kunahitaji wewe uanze kujishughulisha na mambo hayo mara moja wala usisite site.Jambo baya kwako ni kuwa kama kuna mgonjwa hapo nyumbani kwako, lakini kama kuna mjamzito basi atazaliwa mtoto wa kike

MBUZI - CAPRICORN (DES 22 – JAN 20)
Mambo yote unayoyataka yatatimia kati ya leo na Jumatano au Jumamosi ijayo usiku. Pengine katika mwezi wa machi,Tegemea kujionea mambo mengi ambayo ulikuwa umefichwa kwa muda mrefu na watu wako wa karibu. Ili kuleta baraka leo nenda kawatembelee wazee wako.

0 comments:

Post a Comment