Friday, February 7, 2014

JERSON TEGETA AMRUDIA MUNGU

Mshambuliaji wa klabu ya Yanga Jeryson Tegeta hivi karibuni ameamua kumrudia mwenyezi Mungu kwa kuzaliwa upya (kuokoka) baada ya kupata ushuhuda wa
miujiza uliyomkuta mama yake mzazi ambae alikuwa akiumwa na kupata nafuu baada ya Mchungaji Kumuombea.

Tegeta siku za karibuni alikwenda nyumbani kwao Mwanza kwenda kumjulia hali Mama yake mzazi ambae alikuwa anaumwa sana ila kutokana na kupata maombezi aliweza kupata nafuu na hali hiyo ilimsukuma mshambuliaji huyo na yeye kuamua kuokoka baada ya kushuhudia miujiza hiyo kwa mama yake Mzazi.

Niko mwanza nimekuja kumuona mama yangu anaumwa sana bt kaja mchungaji kamuombea mama kapata nafuu kabisa mungu nimkubwa sana na maisha ukimkabidhi mungu kila kitu kinawezekana maisha ya kidunia hayana maana bila yesu nimeokoka rasmi get wel soon mama”



0 comments:

Post a Comment