Friday, February 7, 2014

LULU KUANZA KUJIBU MASHTAKA YA KU UA BILA KUKUSUDIA FEBRUARY 17

Msanii wa filamu Elizabeth Michael Kimemeta (18), maarufu kama Lulu anayekabiliwa na kesi ya mauaji ya bila kukusudia ya msanii mwenzake, Steven
Kanumba (28), anatarajia kupanda kizimbani Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam Februari 17, mwaka huu kujibu mashtaka yake kwa mara ya kwanza.

kesi ya Lulu itasikilizwa mbele ya Jaji Rose Teemba na mshtakiwa atajibu mashitaka yake kama ni kweli au siyo kweli.

Mapema Januari 29, mwaka jana, Lulu aliachiwa kwa dhamana baada ya kesi hiyo kubadilishwa hati ya mashtaka kutoka kwenye kesi ya mauaji kwenda mauaji ya bila kukusudia.


Jaji Mruke alisema kosa linalomkabili mshakiwa lina dhamana kisheria na kwamba mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana kwa kufuata masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao ni watumishi wa serikali watakaosaini hati ya dhamana ya Sh. milioni 20 kila mmoja.

"Tukubaliane wote kwamba hakuna ubishi roho ya mtu imepotea hivyo sheria lazima ifuatwe... pia mshtakiwa awasilishe hati zake za kusafiria, kuripoti kila tarehe Mosi ya mwezi kwa Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na asitoke nje ya Mkoa wa Dar es Salaam bila kibali cha msajili huyo," alisema Jaji Mruke.

Katika kesi ya msingi, Lulu anadaiwa kuwa Aprili 7, mwaka juzi Vatican, Sinza jijini Dar es Salaam, mshtakiwa alimuua Kanumba bila kukusudia.

0 comments:

Post a Comment