Monday, February 10, 2014

HISIA KUJA NA MAWAZO IJUMAA HII

Mwanamuziki Hisia ambae alikuwa akiwakirisha Tanzania na mshindi wa nne katika mashindano la Tusker Project Fame kwa mwaka 2013 anatambulisha
ngoma yake mpya Valentine hii.

Hisia amefunguka na kusema kuwa wimbo wake huo wa Mawazo ameufanyia nchini Kenya ambako ndipo muda mwingi amekuwa akifanya shughuli zake za muziki.

Valentine's Day,natambulisha ngoma yetu ya pili iitwayo Mawazo...coming straight to you kwa mara ya kwanza kabisa... #Hisia #teamhisia #teamtanzania #upcomingsingle #mawazo #hisia #goodmusic”

Hisia anatambulisha wimbo wa pili baada ya ngoma yake ya kwanza Just for you (kwa ajili yako) kufanya poa kwa wakati wake na kuweza kumtambulisha katika soko la muziki wa afrika mashariki.

0 comments:

Post a Comment