Monday, February 10, 2014

WATU PORI ,GHETO BOYS NA AFANDE SELLE KUKINUKISHA MORO

Wasanii kutoka pande za Morogoro ambao walikuwa chini ya King Afande Selle watafanya show siku ya Valentine day katika viwanja vya Rock Garden morogoro
mjini.

Afande sele amesema kuwa watakutana wanamuziki wa Morogoro na baadhi ya wasanii kutoka nje ya Morogogoro na kufanya show hiyo kwa lengo la kutoa burudani kwa Mashabiki wao.

Afande aliongeza kuwa atatumia fursa hiyo kutambulisha wimbo mpya unaokwenda kwa jina la MSHENGA kama zawadi ya pekee na elimu kwa wapendanao wenye mipango mikubwa na malengo ya kuishi pamoja.

Ni kweli tutakuwa na Show BAAB KUBWA' kutoka kwa wasanii wakali wa ndani na nje ya moro nikiwemo mimi mwenyewe Afande Sele The King na timu nzima ya Watu Pori&Gheto Boyz,bila kusahau disko'taamu'toka kwa maDj wa nguvu kuanzia saa kumi jioni mpaka usiku mnene.”

Karibuni saana'wanandugu'kushuhudia nyimbo kibao za sasa na zamani bila kusahau siku hiyo tutambulisha wimbo mpya uitwao'Mshenga'kama zawadi ya kipekee na elimu kubwa kwa Wapendanao kwa dhati na wenye malengo ya kuishi pamoja milele/daima,,,

0 comments:

Post a Comment