Friday, December 20, 2013

NYOTA YAKO LEO IJUMAA TAREHE 20/12/2013:

MSHALE - SAGITARIUS ( NOV 23 - DES 21)
Mchana wa leo uwe na tahadhari, naona kuna taabu na magomvi, utalaumiwa au utapata habari za ugonjwa ambazo zitakutatiza. Wiki hii Kuna ishara ya kupata mali au fedha kutoka kwa mtu wa mbali au kukabidhiwa mali ya watu uitunze. Lazima katika mambo yako uwashirikishe ndugu zako ndio utafanikiwa.

MBUZI - CAPRICORN (DES 22 – JAN 20)
Leo kuna dalili yakupata mali au kupewa pesa au kulipwa deni lako na watu uliokuwa umewafanyia kazi siku za nyuma ambao walikataa kukulipa. Kuna mpango wa safari uliokuwa unausubiri, mpango huo utafunguka baada ya siku tatu kuanzia leo.

NDOO –AQUARIUS (JAN 21 – FEBR 19)
Wiki hii mtoto wako ataugua na kuvuruga mipango yako na utavunjiwa heshima na rafiki yako ambaye hana heshima au wewe utapata maradhi ya kuumwa na kichwa. Kuepusha hayo safiri mbali kwa muda wa wiki.

SAMAKI – PISCES (FEB 20- MACH 20)
Kwanza ujue kuwa safari uliyopanga kwenda ni mbaya na yule mgonjwa yupo ndani ya shida kubwa. Ukitaka kupata mafanikio kwanza msaidie huyo mgonjwa atoke katika matatizo yake ndio utafanikiwa.Tegemea kuletewa zawadi kutoka kwa rafiki yako aliye mbali.

PUNDA- ARIES (MACH 21- APR 20)
Leo kuna dalili kwamba mambo yako mengi yatafanikiwa kwa kuwatumia watu wengine bila ya wewe mwenyewe kushiriki. Leo tegemea kukutana na mtu mkubwa Serikalini ambaye atakusaidia au fanya mipango ya kukutana na wakubwa.

NG’OMBE – TAURUS (APR21 – MAY 20)
Wiki hii maisha yako yatakuwa mazuri, maradhi au matatizo yako madogo madogo yatapungua. Vilevile Mkeo au mumeo atakufurahia kwa zawadi utakayompa. Au toa zawadi kwa uwapendao mambo yako yatafunguka.

MAPACHA - GEMINI (MAY 21- JUN 21)
Mchana wa leo utapokea habari za kutatanisha kuhusu kazi yako au mambo yako ambayo yalikuwa yanakutatiza, Jaribu kuwa na subia usiyaguise mambo hayo yanaweza kuleta matata., unashauriwa usianzishe biashara ya aina yeyote kwa wakati huu.

KAA - CANCER (JUN 22- JUL 22)
Mchana wa leo kuna kila dalili kuwa mambo yako yatafuatiliwa na watu bila ya wewe mwenyewe kujua, jaribu kuwa mwangalifu kwa kila hatua utakayoichukua. Kuna mtu unayemuamini sana unatakiwa uwe muangalifu naye anaweza akakudhuru.

SIMBA - LEO (JUL 23 –AUG 22)
Mchana wa leo kuna kila ishara ya kukwama kwa mipango yako ya kipesa, mipango ya ndoa au mapenzi itaendelea kama kawaida, Kuna mwanamme mrefu mweusi ukikutana naye leo au wiki hii hiyo itakuwa ni dalili ya kufanikiwa kwa kila jambo lako.

MASHUKE - VIRGO (AUG 23- SEPT 23)
Leo kuna dalili kuwa mambo yako hayatakuwa safi na utahadhari unaweza kugombana na kila mtu kazini zu kwenye biashara zako au mtaani kwenu. Wiki hii Jitahidi kuandaa tafrija na uwakirimu watu ili upate baraka na mikosi ikuondoke.

MIZANI - LIBRA (SEPT 24- OCT 23)
Leo kuna dalili ya kuingiliwa katika kazi zako au kusimamishwa kufanya yale uliyokuwa umeyapanga kuyafanya. Vilevile kuna dalili ya kukimbiwa na Mpenzi wako, unashauriwa kuwa mpole na mwenye subira ili ufanikiwe.

NGE - SCORPIO (OCT 24- NOV 22)
Leo naona unafikiria sana mambo ya kushirikiana na mtu katika kazi na kipato, fanya hivyo. Ipo dalili kuwa mambo yako yatafunguka na mikosi kuondoka. Unashauriwa usijaribu kuingia katika biashara inayoendeshwa na ndugu yako.

0 comments:

Post a Comment