Tuesday, November 12, 2013

KAMA UNAKIPAJI IWEJE UFE NA NJAAAA?

Huu ni msemo ambayo alishawahi kuutumia nguli wa muzuki wa Hip Hop Tanzania Prof Jay ambaye kwa sasa anakitumia kipaji chake kuendesha maisha
yake na kujenga misingi mizuri ya kunufaika kutokana na kipaji alichokuwa nacho.
 
Katika kuliona suala Hili msaniii mwingine wa Hip Hop Nash Mc ambaye kwa sasa yeye aliamua kuuza Mix Tape zake katika Mikoa mbalimbali ameamu kuweka wazi msimamo wake kuwa hataweza kutoa nyimbo zake bure kwa mashabiki bali kama wanakubali kazi zake wanapaswa kununua CD hizo ili mwisho wa siku asife njaa na kipaji chake kama ambavyo imewakuta wasaniii wengine wengi tu.
kwa wale washabiki wanaonitumia ujumbe ktk namba zangu,whats app wakiomba niwatumie nyimbo zangu bure,narudia kuwaambia tena,hakuna wimbo wa nash mc utakaopatikana bure mtandaoni,kama ktk watu 9,163 wamekosekana 2000 tu wa kununua cd zangu,bora ya kuuza kila wimbo wangu ili nipate japo kidogo ya jasho langu”
Nategemea kipaji changu kibadli maisha yangu na kweli kazi zinatoka cd zinatangazwa hapa na namna zinatolewa lkn watu wanaulizia wimbo wa bure,kama tumeshindwa kununua cd basi subiri labda nyimbo zivuje lkn cha bure kutoka kwangu hakuna tena! Profesa jay alisema,kama una kipaji iweje ufe na njaaa??!??


0 comments:

Post a Comment