Wakati
mabingwa wa ligi kuu ya Bara, Yanga jana walitua kisiwani Pemba kwa
ajili ya maandalizi ya mechi yao dhidi ya Simba.
Wekundu wa Msimbazi
wao wamehamisha kambi kutoka Bamba Beach na kwenda Bagamoyo.
Kocha msaidizi wa Yanga, Fred Minziro jana alifunguka kwa njia ya Simu na kusema kuwa kikosi chake kiliwasili Pemba jana kwa ajili ya kambi hiyo.
Kocha msaidizi wa Yanga, Fred Minziro jana alifunguka kwa njia ya Simu na kusema kuwa kikosi chake kiliwasili Pemba jana kwa ajili ya kambi hiyo.
Alisema timu hiyo imeamua
kupiga kambi visiwani humo ili kukwepa usumbufu, ikiwa ni pamoja na
kutaka kuwapa wachezaji nafasi ya kufanya mazoezi kwa uhuru zaidi
tofauti wanapokuwa Dar es Salaam.
"Timu iko vizuri,
wachezaji wote wanaendelea vizuri na mazoezi kwa ajili ya kujiandaa
na mechi hiyo," alisema na kuongeza kuwa wanatarajia
kuwashangaza Simba.
Alisema wachezaji wote sasa wako poa baada ya majeruhi wa muda mrefu Salum Telela naye kurejea mazoezini.
Kwa upande wa Simba Kocha
msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' alisema jana kuwa Simba
ambayo imekuwa kambini Bamba Beach, Kigamboni imehama mahala hapo na
kwenda Bagamoyo jana jioni.
Julio alisema Yanga watakiona cha moto
katika mechi hiyo kwenye Uwanja wa Taifa.
0 comments:
Post a Comment